Mashtaka watakiwa kutekeleza maagizo ‘Mpemba wa Magufuli

MAHAKAMA ya Hakimu
Mkazi Kisutu imetoa siku sita kwa upande wa mashitaka katika kesi ya
kujihusisha na biashara haramu ya meno ya tembo inayomkabili
mfanyabiashara Yusuf Ali “Mpemba wa Magufuli” kutoa taarifa ya
utekelezaji wa maagizo, likiwemo la Mkurugenzi wa Mashitaka nchini
(DPP).
Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba alitoa
amri hiyo jana baada ya Wakili wa Serikali, Elizabeth Mkunde kudai kuwa
kesi hiyo imekuja kwa ajili ya kutajwa na kwamba upelelezi umekamilika.
Pia alidai kuwa wapo katika utekelezaji wa
maelekezo waliyopewa na DPP. Wakili wa Utetezi, Nehemia Nkoko alidai
kuwa ahadi za upande wa mashitaka katika kesi hiyo ni za kawaida, hivyo
wanaomba kujua washitakiwa hao watasomewa lini maelezo ya mashahidi.
Hata hivyo, Hakimu Simba alisema mpaka
wiki ijayo wawe wameeleza kesi hiyo imefi kia wapi na kuahirisha kesi
hiyo hadi Julai 24, mwaka huu kwa ajili ya kutajwa. Julai 5, mwaka huu,
upande wa mashitaka uliieleza mahakama kuwa wanalifanyia kazi jalada la
kesi hiyo baada ya kupewa maelekezo na DPP.
Mbali na Yusuph, washitakiwa wengine
katika kesi hiyo ni Charles Mrutu, mkazi wa Mlimba, Morogoro, Benedict
Kungwa wa Mbagala Chamazi, Jumanne Chima wa Mbezi, Ahmed Nyagongo,
dereva na Pius Kulagwa. Washitakiwa kwa pamoja wanakabiliwa na mashitaka
manne ya kujihusisha na biashara haramu ya meno ya tembo yenye thamani
ya Sh milioni 785.6 na upelelezi wa kesi hiyo umekwishakamilika.
Inadaiwa katika tarehe tofauti kati ya
Januari, 2014 na Oktoba, 2016 wakiwa Dar es Salaam, Tanga, Iringa na
Mtwara, walijihusisha na mtandao wa ujangili kwa kukusanya na kuuza
nyara za serikali ambazo ni vipande 50 vya meno ya tembo vyenye thamani
ya dola za Marekani 180,000 (Sh milioni 392.8) bila kibali cha
Mkurugenzi wa Wanyamapori.
Comments
Post a Comment