Janga la Yanga si la Kitoto
JANGA linaonekana kuendelea kuwakabili wawakilishi pekee wa Tanzania kwenye michuano ya kimataifa, Yanga yenye maskani yake Jangwani, Dar es Salaam. Yanga ambao kwa sasa wanaonekana kutokuwa sawa kiuchumi na kiuongozi pia wamekuwa hawapati matokeo mazuri katika mechi zao za kimataifa. Mabingwa hao wa msimu wa mwaka 2016/17 walipata tiketi ya kuiwakilisha nchi mwaka huu kwenye michuano ya kimataifa wakishiriki Ligi ya Mabingwa Afrika. Mambo hayakuwa mazuri kwao kwani walishindwa kuhimili vishindo vya wababe waliokutana nao kwenye michuano hiyo na kujikuta wakitolewa hatua ya kwanza. Kutokana na kufika hatua hiyo kanuni ya Shirikisho la Soka Afrika (Caf) inayosimamia michuano hiyo ikawaruhusu kuangukia kwenye hatua ya mtoano ya Kombe la Shirikisho Afrika ambapo huko walipambana hadi wakafanikiwa kuvuka hatua hiyo mpaka kwenye makundi. Kwenye makundi wamepangwa kundi D pamoja na timu za USM Alger ya Algeria, Rayon Sports ya Rwanda pamoja na Go
Comments
Post a Comment